Tuesday 27 December 2016

MCHUNGAJI JOSEPHNE MILLER KUTOKA MAREKANI AFURAHIA KUTEMBELEA HIFADHI YA TAIFA SERENGETI.

Disemba 19 hadi 25 mwaka huu, Mchungaji Josephine Miller (wa tatu kushoto) kutoka Marekani alikuwa akifundisha na kuhubiri katika Kanisa la EAGT Lumala Mpya Jijini Mwanza. 

Baada ya huduma hiyo, jana Disemba 27, wenyeji wake (pichani) wakiongozwa na Mchungaji Kiongozi wa Kanisa hilo, Dkt.Daniel Moses Kulola (wa sita kulia) na Mama Mchungaji Mercy Kulola (wa tano kulia), walimtembeza Mchungaji Miller katika hifadhi ya Taifa Serengeti ili kujionea vivutio mbalimbali vilivyopo katika fidhahi hiyo.
Imeandaliwa na George Binagi, Picha na Jorum Samwel
Wanaumini wa Kanisa la EAGT Lumala Mpya Jijini Mwanza, baada ya kuwasili katika hifhadhi ya Serengeti
Waumini wa EAGT Lumala Mpya wakifurahia uwepo wao ndani ya hifadhi

Sunday 25 December 2016

MWIMBAJI MAARUFU WA KANISA LA EAGT LUMALA MPYA JIJINI MWANZA AFUNGA PINGU ZA MAISHA.

Mbali ya kuwa Sikukuu ya Krismasi kwa Wakristo duniani, pia jana Disemba 25,2016 ilikuwa siku ya furaha kwa ndugu, jamaa na marafiki wa Bwana harusi Mathew Akrama Rwekila na Bibi harusi Agnes Martine (wawili katikati), baada ya kufunga pingu za maisha katika Kanisa la EAGT Lumala Mpya Jijini Mwanza.

MCHUNGAJI JOSEPHINE MILLER KUTOKA MAREKANI AZUNGUMZIA SIKUKUU YA CHRISMASI.

Mchungaji Josephine Miller (kushoto) kutoka nchini Marekani, akizungumza na George Binagi (kulia), baada ya kuhitimisha mafundisho na mahubiri ya juma zima katika Kanisa la EAGT Lumala Mpya hii leo.

Amesema Krismasi ni msimu muhimu si tu kwa Amerika bali pia kote ulimwenguni hususani kwa wote wanaomwamini Yesu Kristo aliyezaliwa Bethlehem. Anasema kuzaliwa kwa Yesu Kristo ilikuwa ni zawadi kutoka kwa Mungu kwa ajili yetu.

Amewatia moyo watanzania kumwamini Mungu kwani yuko pamoja nao, bila kujalisha hali yoyote ile waliyonayo ikiwemo kiuchumi.
Bonyeza HAPA Au play kusikiliza

IBADA MAALUMU YA KRISMASI, KANISA LA EAGT LUMALA MPYA LABARIKI WATOTO.

Mchungaji Kiongozi wa Kanisa la EAGT Lumala Mpya lililopo Sabasaba Jijini Mwanza, Dkt.Daniel Moses Kulola, hii leo Disemba 25, 2016 akihubiri kwenye ibada maalumu ya Krismasi ambayo imeenda sambamba na kubariki watoto ikiwa ni ishara njema katika siku hii ya kuzaliwa kwa Yesu Kristo. Somo limetoka Kitabu cha Marko Mtakatifu 10:07.

Ibada hiyo...

Sunday 20 November 2016

PICHA YA MAREHEMU ASKOFU DR.MOSES KULOLA NA ALIYEKUA SPIKA MSTAAFU MAREHEMU SAMUEL SITTA WALIPOKUTANA

Katika kuonesha kuwakumbuka watu hawa muhimu katika Tanzania, mtoto wa aliyekua Askofu Mku wa kanisa la EAGT nchini Tanzania Dr.Moses Kulola, afahamikaye kama Mchungaji Dr. Daniel Kulola amepost katika ukurasa wake wa mtandao wa Facebook picha akiwa na baba yake "Kulola " na aliyekua Spika Mstaafu marehemu Samuel Sitta siku walipokutana pamoja uwanja wa ndege katika safari .
Itakumbukwa kuwa Askofu Moses Kulola alifariki dunia mwaka 2013 akiacha alama kama Baba wa Injili nchini Tanzania na kiongozi aliyewalea kihuduma watumishi wengi wakubwa na maarufu , huku aliyekua Spika mstaafu Samuel Sitta amefariki mwezi November mwaka huu 2016 na kuacha simanzi nzito kwa taifa kutokana na mchango wake mkubwa alioutoa kwa taifa la Tanzania katika utumishi wake katika serikali.

Thursday 17 November 2016

MCHUNGAJI DR.DANIEL MOSES KULOLA ASHEREHEKEA MIAKA 27 YA NDOA YAKE

 Mchungaji wa Kanisa la EAGT Lumala Mpya jijini Mwanza leo ametimiza miaka 27 ya ndoa na mke wake Bi.Mercy Kulola baada ya kuwa pamoja tangu walipofunga ndoa mwaka 1989.

Katika ukurasa wake wa facebook Dr.Kulola amesema kuwa anamshukuru Mungu kwa neema na rehema zake alizowajalia katika ndoa yao, huku akielekeza salamu zake za upendo kwa mkewe na msaidizi katika huduma ya uinjilist ambayo wamekua wakiifanya kwa kuzunguka nchi mbalimbali kuhubiri injili katika mikutano ya hadhara na mikutano ya ndani.

Katika ukurasa wake hiki ndicho alichokiandika Mchungaji Dr.Kulola jr.


ATTENTION PLEASE
Today 18th Nov, is our marriage anniversary, We thank God for His aboundant Grace mercy, and honor in our marriage. You can imaging since 1989 until today 18th Nov 2016 it is by the Grace of God. Let me tell my lovely wife Mercy Daniel that you are everything to me, ilove you, and respect you. Share with us please to say anything


 
 
 


 

MAHUBIRI YA MCH.DR.DANIEL MOSES KULOLA HUKO QUEBEC CANADA


Sunday 13 November 2016

KANISA LA EAGT LUMALA MPYA JIJINI MWANZA LAFANYIKA BARAKA KWA WAUMINI WAKE.

 Waumini wa Kanisa la EAGT LUMALA MPYA Jijini Mwanza, wakipata mahubiri, maombi na mafundisho ya mchungaji wa kanisa hilo, Dkt.Daniel Moses Kulola, katika ibada za jana jumapili, Novemba 13,2016.

Mtumishi huyu amefanyika...

Tuesday 8 November 2016

MUUMINI WA KANISA LA EAGT LUMALA MPYA JIJINI MWANZA ASHUHUDIA UKUU WA MUNGU BAADA YA KUIBUKA MILIONEA NA M-POWER.

Mshindi wa shilingi Milioni 100 kutoka Jijini Mwanza katika promosheni ya M-Power inayosimamiwa na kampuni ya simu ya Vodacom, Mama Paulina Kulwa (kushoto), akiwa na mchungaji wa Kanisa la EAGT Lumala Mpya, Dkt.Daniel Moses Kulola wakati wa kukabidhiwa hundi yake.

Mama Paulina Kulwa (58) ni...

Sunday 6 November 2016

MAFUNDISHO YA MCHUNGAJI DANIEL KULOLA KUONESHWA KWENYE KING'AMUZI CHA CONTINENTAL.

Usikose kufuatilia mahubiri na mafundisho ya Mchungaji wa Kanisa la EAGT Lumala Mpya lililopo Sabasaba Ilemela Jijini Mwanza, Dkt.Daniel Moses Kulola (kulia), kwenye runinga ya STAR RELIGION kupitia king'amuzi cha CONTINENTAL.

Ni kila siku za...

Saturday 22 October 2016

HUDUMA YA MCHUNGAJI DANIEL KULOLA WA KANISA LA EAGT LUMALA MPYA JIJINI MWANZA YAFANA MKOANI DODOMA.

Huduma ya injili iliyofanywa na mchungaji kiongozi wa Kanisa la "EAGT Lumala Mpya Internationa Church " lililopo Sabsaba Ilemela Jijini Mwanza, Dkt.Daniel Moses Kulola (pichani), mkoani Dodoma imekuwa ya kufaana na watu wengi wameokoka na kubarikiwa.

Ni katika mkutano wa...

Thursday 20 October 2016

CHURCH BIBLE STUDIES IN OUR CHURCH- GOING DEEPER IN KNOWING GOD






MCHUNGAJI WA KANISA LA EAGT MITO YA BARAKA JIJINI DAR ES SALAAM AHUDUMU KATIKA KANISA LA EAGT LUMALA MPYA JIJINI MWANZA.

Mchungaji  Bruno Mwakibolwa kutoka Kanisa la EAGT Mito ya Baraka Temeke Jijini Dar es salaam, jumapili iliyopita Oktoba 16, 2016 alihudumu katika Kanisa la EAGT Lumala Mpya la Sabasaba Ilemela Jijini Mwanza, baada ya kuwasili katika kanisa hilo akitokea nchini Kenya.

Ilikuwa Ibada iliyojaa...

Sunday 16 October 2016

MCHUNGAJI KULOLA ARINDIMA KWENYE HITIMISHO LA MKUTANO MKUWA WA INJILI KANISA LA EAGT POSTA B MABATINI JIJINI MWANZA.

Mchungaji Kiongozi wa Kanisa la EAGT Lumala Mpya lililopo Sabasaba Ilemela Jijini Mwanza, Dkt.Daniel Moses Kulola (pichani), kwa siku tatu mfululizo hadi jana jumapili Oktoba 16, 2016 alihudumu katika Kilele cha Mkutano Mkubwa wa Injili uliofanyika Kanisa la EAGT Posta B, Mabatini Jijini Mwanza, uliofanyika kwa juma zima kuanzia Oktoba 09 hadi Oktoba 16 mwaka huu.

Ulikuwa Mkutano uliojaa Neema ya Mungu ambapo...

Sunday 9 October 2016

TAMASHA LA KUSIFU NA KUABUDU KATIKA KANISA LA EAGT LUMALA MPYA JIJINI MWANZA LAFANA.

Jana Jumapili Oktoba 09, 2016 kuanzia majira ya saa nane mchana hadi saa 12 jioni kulifanyika Tamasha Kubwa la Kusifu na Kuabudu, katika Kanisa la Kimataifa la EAGT Lumala Mpya lililopo Sabasaba Manispaa ya Ilemela Jijini Mwanza.

Mamia ya watu/waumini...

Thursday 6 October 2016

TAMASHA KUBWA LA KUSIFU NA KUABUDU KUFANYIKA KATIKA KANISA LA EAGT LUMALA MPYA JIJINI MWANZA.

Jumapili Oktoba 09, 2016 katika Kanisa la "EAGT Lumala Mpya International Church" Sabasaba Manispaa ya Ilemela Jijini Mwanza, linatarajiwa kufanyika tamasha kubwa la Kusifu na Kuabudu.
Mchungaji Kiongozi wa Kanisa hilo...

Thursday 29 September 2016

MCHUNGAJI DKT.DANIEL KULOLA KURINDIMA KWENYE MKUTANO MKUBWA WA INJILI JIJINI MWANZA.


Kanisa la EAGT Posta “B” Mabatini Jijini Mwanza chini ya Mchungaji Lameck Nkumba, linawakaribisha watu wote kwenye mkutano mkubwa wa injili utakaofanyika katika viwanja vya kanisa hilo vinavyotizamana na geti la polisi Mabatini nyuma ya iliyokuwa Orange Tree Hotel.

Mhubiri wa kitaifa na kimataifa ambaye amehubiri mataifa mbalimbali duniani ikiwemo Marekani, Canada, Uingereza, Ireland, Wales , Scotland, Ujerumani, Dernmark, Swirtzland, Afrika Kusini, DRC Congo na mengine mengi, Dkt.Daniel Moses Kulola (pichani), atahudumu kwenye mkutano huo akishirikiana na wahubiri wengine.

Ni wiki moja yenye miujiza na uponyaji wa nguvu ya Mungu, kuanzia jumapili tarehe 9.10.2016 hadi jumapili tarehe 16.10. 2016 muda ni kuanzia saa 9.00 mchana hadi saa 12 jioni, kila siku.

Waimbaji mbalimbali akiwemo Mwanyamaki kutoka Morogoro, Emannuel Mgogo kutoka Dar es salaam pamoja na kwaya zinatotamba Jijii Mwanza kama vile Havillah Gospel Singers kutoka EAGT Lumala Mpya, na kwaya ya EAGT Posta “B” zitahudumu kwenye mkutano huo.

Ewe baba, mama, kaka, dada, ndugu, jamaa na marafiki, fika kwenye mkutano huo ili ukutane na nguvu ya Mungu ambapo wagonjwa mbalimbali, wenye mapepo, mikosi na waliofungwa na vifungo vya ibirisi watafunguliwa kwa jina la Yesu, bila malipo.
Kwa msaada wa Kiroho, piga simu nambari 0784 43 77 82 
Bonyeza HAPA Kusikiliza, Au Bonyeza Play hapo chini .

Monday 5 September 2016

ILIVYOKUWA KWENYE USIKU WA BWANA BALIYANGA NA MISS PENINA KANISA LA EAGT LUMALA MPYA JIJINI MWANZA.


Jana Septemba 04, 2016 ilikuwa siku njema kwa waumini wa Kanisa la EAGT Lumala Mpya Jijini Mwanza, Bwana Robson Mkesha Baliyanga na Miss Penina Mkama, baada ya kufunga ndoa takatifu katika Kanisa la EAGT Lumala Mpya Jijini Mwanza, chini ya Mchungaji Kiongozi Dkt.Daniel Moses Kulola.

Sunday 4 September 2016

BWANA ROBSON BALIYANGA NA MISS PENINA MKAMA WA EAGT LUMALA MPYA JIJINI MWANZA WAFUNGA PINGU ZA MAISHA.

Waumini wawili wa Kanisa la EAGT Lumala Mpya lililopo Sabsaba Ilemela Jijini Mwanza, Bwana Robson Mkesha Baliyanga (katikati) na Miss Penina Mkama (kushoto) leo Septemba 04,2016, wamefunga ndoa (pingu za maisha) takatifu.

Ibada ya ndoa hiyo imefanyika katika Kanisa hilo na kuuongozwa na Mchungaji Kiongozi, Dkt.Daniel Moses Kulola. Tafrija inafanyika jioni kwenye ukumbi wa Maendeleo House uliopo Iloganzara Jijini Mwanza.

"Mungu akasema;

Saturday 27 August 2016

KANISA LA EAGT LUMALA MPYA JIJINI MWANZA KUFANYA HARAMBEE YA UJENZI WA KANISA JIPYA NA LA KISASA.


Kanisa la EAGT Lumala Mpya lililopo Sabasaba Ilemela Jijini Mwanza, chini ya Mchungaji kiongozi, Dkt.Daniel Moses Kulola, linapenda kuwakaribisha watu wote kwenye Harambee ya Ujenzi wa Kanisa jipya na la kisasa linalotarajiwa kujengwa katika viwanja vya kanisa hilo.

MCHUNGAJI DANIEL KULOLA AKUTANA NA MTOTO MTANZANIA ALIEIGIZA SINEMA YA "THE REAL MVP" NCHINI MAREKANI.

Mchungaji Kiongozi wa Kanisa la EAGT Lumala Mpya lililopo Sabasaba Jijini Mwanza, Dkt.Daniel Moses Kulola (kushoto) amekutana na mtoto mtanzania aliyeigiza sinema ya The Real MVP nchini Marekani.

Dkt.Kulola alikutana na mtoto huyo, Evan Byarushengo (7 kulia), alipokuwa Texas nchini Marekani kwa ajili ya huduma ya neno la Mungu ambapo Mchungaji Kulola amewasili leo Jijini Mwanza.
Mtoto huyo (kulia) amekuwa miongoni mwa watoto wachache duniani hususani kutoka mataifa ya Afrika, kuweza kushiriki katika sinema za Hollywood nchini Marekani akiwa na Mastaa mbalimbali.
Mchungaji Kulola akiwa pamoja na wafamilia ya mtoto huyo nchini Marekani.

Monday 22 August 2016

MCHUNGAJI DANIEL KULOLA WA KANISA LA EAGT LUMALA MPYA JIJINI MWANZA AKIHUDUMU NCHINI MAREKANI.

Mchungaji Kiongozi wa Kanisa la EAGT Lumala Mpya lililopo Ilemela Jijini Mwanza, Dkt.Daniel Moses Kulola (pichani) yuko nchini Marekani kwa huduma ya kiroho tangu jumanne iliyopita Agost 16,2016 ambapo alianza kuhudumu ijumaa Agost 19,2016 katika Kanisa la "Assemblies Of God Agape Church" lililopo Boston Marekani.

Huduma ya Mchungaji Dkt.Kulola inaendelea katika majimbo mbalimbali nchini Marekani ikiwemo Dallas, Texas, Houston na Arizona.

Aidha Mchungaji Kulola ametoa shukurani zake za dhati kwa familia yake, Kanisa la EAGT Lumala Mpya, ndugu, jamaa pamoja na marafiki kwa kuendelea kumuombea kwa huduma anayoifanya nchini Marekani ambapo watu wengi wanaokoka na kuponywa.
Mchungaji Dkt.Daniel Kulola, akihudumu nchini Marekani.
Picha ya pamoja baada ya huduma katika jimbo la Boston
Mchungaji Kulola (katikati) na familia yake
Mchungaji Dkt.Daniel Kulola (kushoto), akiwa na Mama Mchungaji, Mercy Kulola(kulia).
Bonyeza HAPA Kwa Taarifa Zaidi

Friday 5 August 2016

MCHUNGAJI DKT.DANIEL KULOLA WA KANISA LA EAGT LUMALA MPYA MWANZA KUITETEMESHA INJILI KWA MARA NYINGINE NCHINI MAREKANI.

Mchungaji wa Kanisa la EAGT Lumala Mpya la Jijini Mwanza, akihubiri katika moja ya mikutano yake iliyofanyika mkoani Morogoro.

Friday 29 July 2016

PASTOR DANIEL MOSES KULOLA OF EAGT LUMALA MPYA MWANZA TO VISIT USA.

Greetings my friend, Again God has given to me a chance to come to America, this time i wont stay in USA for long time it is just for 2 weeks then i come back home Tanzania.

My schedule will be in Boston from 9th to 14th August then 15th August to Dallas, Houston to 22nd, on 23rd to Arizona. my ticket back to Tanzania reads on 25th from Arizona to Boston and Boston to Tanzania.
I thought it is good to let you know so that you can pray for me and also call me for greetings.

Saturday 30 April 2016

THE MISSION HERE IN CANADA

I thank GOD that He helped to connect me with the people in Canada.
1. My host pastor Fred Mitched with his wife
2. Pastor Bob of Global kingdom ministries in Toronto
3. Pastor Domitila Nabibone in Ottawa
4. Pastor Jonathan Esongo in Montreal
The mission though is still on the marathon but already have seen the wonderful hand of God with me and my wife
 

Sample text

Welcome note

Dear our Brethren in Jesus Welcome to our website. We are so glad that you have chosen to visit our site. On this site you will be able to know us, our values and challenges as a church family, activities and our weekly and even Yearly program and what the Lord is doing through us here in EAGT Lumala mpya church , Mwanza, Tanzania. Our prayer is that as you browse through this website, the Lord will speak to you so that you may partner with us in prayer and any other way that He may lead you to. Let us join hands as we seek to fulfill the mission and vision that God has given us. Let us redeem the time, before the Lord of times returns. Again welcome. Yours in God’s service, Pastor Dr. Daniel Moses kulola.

Sample Text

 
Blogger Templates