Monday 26 June 2017

MERCY BAND KUTOKA MAREKANI WATIKISA NDANI YA EAGT LUMALA MPYA.

Waimbaji kutoka Marekani jana jumapili Juni 25,2017  wamerindima kwenye tamasha zuri la Kusifu na Kuabudu katika kanisa la kimataifa la EAGT Lumala Mpya lililopo nyuma ya Soko Kuu la Sabasaba Jijini Mwanza.

Mbali na waimbaji hao wanaounda kundi la Mercy Band, pia walikuwepo waimbaji kutoka EAGT Lumala Mpya waliojaaliwa karama ya kusifu na kumwabudu Mungu kwa Roho na Kweli na hivyo kufanya tamasha hilo kuwa la kipekee.

Waumini wa kanisa la EAGT Lumala Mpya wakiongozwa na mchungaji wao, Dkt.Daniel Moses Kulola walifurahishwa na tamasha hilo huku kila mmoja akivutiwa namna waliookoka wanavyomtumikia Mungu kwa ari na nguvu.

Baada ya tamasha hilo, unaanza tena mkuano wa OYES (Open Your Eyes and See-Fungua Macho Yako na Uone) ikiwa ni mkutano wa pili mwaka huu ambapo mkutano huo utaanza kesho Juni 27 hadi jumatatu Julai 03 katika viunga vya kanisa la EAGT Lumala Mpya.

Mchungaji Kulola alisema katika mkutano huo, atakuwepo mhubiri Ken Maxwell pamoja na Mercy Band kutoka Florida Marekani bila kuwasahau waimbaji wa nyumbani kama vile Havillah Gospel Singers, Revival Kwaya, Sam D, David Cosmas, Allen Ndageji, Agness Akrama na Happy Shamawere.

Usikose katika mkutano huo wa OYES ambapo kutakuwa na maombezi pamoja na mafundisho ya neno la Mungu.

Sunday 25 June 2017

MUUMINI WETU VICTOR MISANA AMTAMBULISHA MCHUMBA WAKE.

Mdau Victor Misana amemtambulisha na kumvisha pete ya uchumba,  mwezi wake Queen Mrema. Zoezi hilo limefanyika leo Juni 25,2017 katika kanisa la EAGT Lumala Mpya Jijini Mwanza, chini ya mchungaji Dkt.Daniel Moses Kulola. Harusi inatarajiwa kufanyika hivi karibuni.

Tuesday 20 June 2017

HABARI NJEMA KUTOKA KANISA LA EAGT LUMALA MPYA JIJINI MWANZA.

 Injili inatarajiwa kurindima katika viunga vya kanisa la EAGT Lumala Mpya lililopo nyuma ya Soko Kuu  la Sabasaba Jijini Mwanza, kuanzia jumapili ijayo juni 25,2017 kwa kuanza na tamasha la muziki wa injili likiwahusisha waimbaji wa nyumbani na Marekani.

Mchungaji wa kanisa hilo, Dkt.Daniel Moses Kulola amesema tamasha hilo litakuwa la aina yake na kwamba watumishi wa Mungu ambao ni pamoja na Glen Elleben, Garry & Christina, Charity Brading, Dylan Smith & Makayla Rodgers wamethibitisha kuwepo kwenye tamasha hilo, siku ya jumapili.

Dkt.Mchunhaji Kulola ameongeza kwamba baada ya tamasha hilo, utaanza mkuano wa OYES (Open Your Eyes and See-Fungua Macho Yako na Uone) ikiwa ni mkutano wa pili mwaka huu ambapo mkutano huo utaanza Juni 27 hadi Julai 03 mwaka huu katika viunga hivyo vya kanisa la EAGT Lumala Mpya.

Amesema mhubiri Ken Maxwell pamoja na Mercy Band kutoka Florida Marekani watahudumu kwenye mkutano huo wa OYES bila kuwasahau waimbaji wa nyumbani kama vile Havillah Gospel Singers, Revival Kwaya, Sam D, David Cosmas, Allen Ndageji, Agness Akrama na Hapy Shamawere.

Usikose kufika katika tamasha hilo la jumapili pamoja na mkutano wa OYES ambapo kutakuwa na maombezi na mafundisho ya neno la Mungu.

Thursday 1 June 2017

VIDEO: YANAYOJIRI KWENYE MKUTANO WA OYES 2017 JIJINI MWANZA.


Makumi ya wananchi wafunguliwa kwenye mkutano wa Injili wa OYES 2017 (Open Your Eyes and See-Fungua Macho Yako na Uone) kanisa la EAGT Lumala Mpya Jijini Mwanza. 
 

Sample text

Welcome note

Dear our Brethren in Jesus Welcome to our website. We are so glad that you have chosen to visit our site. On this site you will be able to know us, our values and challenges as a church family, activities and our weekly and even Yearly program and what the Lord is doing through us here in EAGT Lumala mpya church , Mwanza, Tanzania. Our prayer is that as you browse through this website, the Lord will speak to you so that you may partner with us in prayer and any other way that He may lead you to. Let us join hands as we seek to fulfill the mission and vision that God has given us. Let us redeem the time, before the Lord of times returns. Again welcome. Yours in God’s service, Pastor Dr. Daniel Moses kulola.

Sample Text

 
Blogger Templates