Sunday 26 February 2017

WAUMINI WA KANISA LA EAGT LUMALA MPYA JIJINI MWANZA WAWATUZA WATUMISHI WA MUNGU KUTOKA CANADA.

Mchungaji wa Kiongozi wa Kanisa la EAGT Lumala Mpya Jijini Mwanza, Dkt.Daniel Moses Kulola, akizungumza kwenye ibada ya jana jumapili kwenye kanisa hilo ikiwa ni siku ya mwisho ya huduma iliyokuwa ikitolewa na watumishi wa Mungu kutoka Canada kuanzia Februari 16,2017.

Kuanzia Februari 16 hadi Februari 21,2017 watumishi hao walikuwa wakitoa semina kwa makundi mbalimbali ikiwemo wajane, wanandoa na vijana ambapo kuanzia februari 22 hadi 24 asubuhi waliendesha zoezi la upimaji wa afya bure na februari 22 hadi 26 kuanzia saa tisa mchana kulikuwa na mahubiri kwa watu wote.

Watumishi wa Mungu kutoka Canada walikuwa ni Fred Mitchell, Karlin Mitchell, Joyce Dickson, Shirleen Weeks, Fredrica Walters na Barry Walters. Katika huduma hiyo pia waimbaji mbalimbali akiwemo Martha Baraka walialikwa kuhudumu.

oKatika ibada ya jana, watumishi wa kanisa la EAGT Lumala Mpya, waliwatunuku zawadi watumishi hao ikiwa ni ishara ya kusema ahsante kwa huduma yao njema.
Waumini wa Kanisa la EAGT Lumala Mpya wakimsikiliza Mchungaji Dkt.Daniel Moses Kulola

Wednesday 22 February 2017

WAIMBAJI WENGI AKIWEMO MARTHA BARAKA WATIKISA MKUTANO WA INJILI JIJINI MWANZA.

Mwimbaji wa muziki wa Injili nchini Martha Baraka (katikati), kwaya na waimbaji mbalimbali wamepamba vyema Mkutano Mkubwa wa Injili unaofanyika Kanisa la EAGT Lumala Mpya Ilemela Jijini Mwanza.

Waimbaji wengine kwenye mkutano huo ni pamoja na Stella Ngumba, Ajuaye Onesmo na kwamba kadhaa ikiwemo EAGT Kaangaye na wenyeji New Salvation na Havilah Gospel Singers.

Watumishi wa Mungu kutoka Canada ambao ni Fred Mitchell, Karlin Mitchell, Joyce Dickson, Shirleen Weeks, Fredrica Walters na Barry Walters kwa pamoja na wenyeji wao chini ya Mchungaji Dkt.Daniel Moses Kulola, wanahudumu katika mkutano huo ikiwemo kufanya maombezi ya nguvu kwa watu wote.

Mkutano huo ulianza jana Februari 22 na utarajiwa kufikia tamati jumapili hii Februari 26,2016 katika viwanja vya kanisa hilo kuanzia saa tisa kamili mchana.
#BMG

WENGI WAJITOKEZA KUPIMA AFYA BURE KANISA LA EAGT LUMALA MPYA JIJINI MWANZA.

Zoezi la upimaji wa Afya Bure kwa wakazi wa Jiji la Mwanza na maeneo jirani linalofanyika kwa siku tangu kuanzia jana, linaendelea katika viwanja vya Kanisa la EAGT Lumala Mpya lililopo nyuma ya Soko Kuu la Sabasaba Ilemela.

Mchungaji wa kanisa hilo, Dkt.Daniel Moses Kulola (kulia) amebainisha kwamba jana zaidi ya wananchi 150 walijitokeza kupima afya zao ambapo zaidi ya 70 walihudumiwa na kurejea nyumba.

Alisema zoezi hilo limejikita kwenye uchunguzi wa afya ya uzazi, kisukari, presha pamoja na uzito likiongozwa na wataalamu wa afya kutoka Canada wanaosaidizana na wataalamu wazawa na muda ni kuanzia saa mbili kamili asubuhi.

Sunday 19 February 2017

WANANCHI WAKARIBISHWA KWENYE VIPIMO VYA AFYA BURE KANISA LA EAGT LUMAPA MPYA JIJINI MWANZA.

Mchungaji wa Kanisa la EAGT Lumala Mpya lililopo nyuma ya Soko Kuu la Sabasaba Ilemela Jijini Mwanza, Dkt.Daniel Moses Kulola, akiwaombea waumini wa kanisa hilo kwenye ibada ya jana jumapili Februari 20,2017.

Kumbuka kuna mwendelezo wa mahubiri na mafundisho kutoka kwa watumishi wa Mungu kutoka Canada katika kanisa hilo kuanzia alhamisi iliyopita Februari 16 ambapo tayari makundi ya akina wanandoa, mama, wajane na vijana wamenufaika na mafundisho hayo.

Mafundisho mengine yanaendelea wiki hii kwa makundi mbalimbali ikiwemo mabinti hadi kesho februari 21 na baada ya hapo itafuata huduma ya vipimo bure pamoja na mahubiri kwa watu wote nje ya viunga vya kanisa hilo.

Thursday 16 February 2017

UJUMBE MKUBWA WA WATUMISHI WA MUNGU KUTOKA CANADA WAPOKELEWA JIJINI MWANZA TAYARI KWA HUDUMA.

Majira ya saa mbili usiku jana, ujumbe mkubwa wa watumishi wa Mungu kutoka nchini Canada waliwasili kwenye uwanja wa ndege wa Jijini Mwanza, kwa ajili ya huduma katika kanisa la EAGT Lumala Mpya lililopo nyuma ya Soko Kuu la Sabasaba Ilemela Jijini Mwanza.

Pichani ni waumini wa Kanisa la EAGT Lumala Mpya wakiongozwa na mchungaji wao Dkt.Daniel Moses Kulola (katikati), waliojitokeza kwenye mapokezi hayo.

Ujumbe wa watumishi wa Mungu kutoka Canada uliongozwa na Mchungaji Fred Mitchel pamoja na Mchungaji Fredrica Walters ambapo huduma ya semina imeanza hii leo Februari 16,2017. 

Kutakuwa na semina na mafundisho kwa makundi mbalimbali ikiwemo akinamama, vijana, wanandoa na wajane hadi Februari 22 na baada ya hapo kutakuwa na mahubiri kabambe hadi Februari 26,2017 katika viunga vya Kanisa la EAGT Lumala Mpya.
#BMG

Sunday 12 February 2017

KUELEKEA KWENYE HARUSI YA KIJANA WETU, GEORGE BINAGI.

Jana jumapili Februari 12,2017, mdau George Binagi ambaye ni Mwanahabari wa Lake Fm Mwanza na Mwanablogu wa Binagi Media Group (kulia), alimtambulisha mchumba wake, Pendo Kisaka, mbele ya waumini wenzake wa Kanisa la EAGT Lumala Mpya lililopo Sabasaba Jijini Mwanza na kutangaza kusudio la harusi inayotarajiwa kufanyika mwezi March mwaka huu.
Picha na Robert Kasamwa
 

Sample text

Welcome note

Dear our Brethren in Jesus Welcome to our website. We are so glad that you have chosen to visit our site. On this site you will be able to know us, our values and challenges as a church family, activities and our weekly and even Yearly program and what the Lord is doing through us here in EAGT Lumala mpya church , Mwanza, Tanzania. Our prayer is that as you browse through this website, the Lord will speak to you so that you may partner with us in prayer and any other way that He may lead you to. Let us join hands as we seek to fulfill the mission and vision that God has given us. Let us redeem the time, before the Lord of times returns. Again welcome. Yours in God’s service, Pastor Dr. Daniel Moses kulola.

Sample Text

 
Blogger Templates