Saturday 27 August 2016

KANISA LA EAGT LUMALA MPYA JIJINI MWANZA KUFANYA HARAMBEE YA UJENZI WA KANISA JIPYA NA LA KISASA.


Kanisa la EAGT Lumala Mpya lililopo Sabasaba Ilemela Jijini Mwanza, chini ya Mchungaji kiongozi, Dkt.Daniel Moses Kulola, linapenda kuwakaribisha watu wote kwenye Harambee ya Ujenzi wa Kanisa jipya na la kisasa linalotarajiwa kujengwa katika viwanja vya kanisa hilo.

MCHUNGAJI DANIEL KULOLA AKUTANA NA MTOTO MTANZANIA ALIEIGIZA SINEMA YA "THE REAL MVP" NCHINI MAREKANI.

Mchungaji Kiongozi wa Kanisa la EAGT Lumala Mpya lililopo Sabasaba Jijini Mwanza, Dkt.Daniel Moses Kulola (kushoto) amekutana na mtoto mtanzania aliyeigiza sinema ya The Real MVP nchini Marekani.

Dkt.Kulola alikutana na mtoto huyo, Evan Byarushengo (7 kulia), alipokuwa Texas nchini Marekani kwa ajili ya huduma ya neno la Mungu ambapo Mchungaji Kulola amewasili leo Jijini Mwanza.
Mtoto huyo (kulia) amekuwa miongoni mwa watoto wachache duniani hususani kutoka mataifa ya Afrika, kuweza kushiriki katika sinema za Hollywood nchini Marekani akiwa na Mastaa mbalimbali.
Mchungaji Kulola akiwa pamoja na wafamilia ya mtoto huyo nchini Marekani.

Monday 22 August 2016

MCHUNGAJI DANIEL KULOLA WA KANISA LA EAGT LUMALA MPYA JIJINI MWANZA AKIHUDUMU NCHINI MAREKANI.

Mchungaji Kiongozi wa Kanisa la EAGT Lumala Mpya lililopo Ilemela Jijini Mwanza, Dkt.Daniel Moses Kulola (pichani) yuko nchini Marekani kwa huduma ya kiroho tangu jumanne iliyopita Agost 16,2016 ambapo alianza kuhudumu ijumaa Agost 19,2016 katika Kanisa la "Assemblies Of God Agape Church" lililopo Boston Marekani.

Huduma ya Mchungaji Dkt.Kulola inaendelea katika majimbo mbalimbali nchini Marekani ikiwemo Dallas, Texas, Houston na Arizona.

Aidha Mchungaji Kulola ametoa shukurani zake za dhati kwa familia yake, Kanisa la EAGT Lumala Mpya, ndugu, jamaa pamoja na marafiki kwa kuendelea kumuombea kwa huduma anayoifanya nchini Marekani ambapo watu wengi wanaokoka na kuponywa.
Mchungaji Dkt.Daniel Kulola, akihudumu nchini Marekani.
Picha ya pamoja baada ya huduma katika jimbo la Boston
Mchungaji Kulola (katikati) na familia yake
Mchungaji Dkt.Daniel Kulola (kushoto), akiwa na Mama Mchungaji, Mercy Kulola(kulia).
Bonyeza HAPA Kwa Taarifa Zaidi

Friday 5 August 2016

MCHUNGAJI DKT.DANIEL KULOLA WA KANISA LA EAGT LUMALA MPYA MWANZA KUITETEMESHA INJILI KWA MARA NYINGINE NCHINI MAREKANI.

Mchungaji wa Kanisa la EAGT Lumala Mpya la Jijini Mwanza, akihubiri katika moja ya mikutano yake iliyofanyika mkoani Morogoro.
 

Sample text

Welcome note

Dear our Brethren in Jesus Welcome to our website. We are so glad that you have chosen to visit our site. On this site you will be able to know us, our values and challenges as a church family, activities and our weekly and even Yearly program and what the Lord is doing through us here in EAGT Lumala mpya church , Mwanza, Tanzania. Our prayer is that as you browse through this website, the Lord will speak to you so that you may partner with us in prayer and any other way that He may lead you to. Let us join hands as we seek to fulfill the mission and vision that God has given us. Let us redeem the time, before the Lord of times returns. Again welcome. Yours in God’s service, Pastor Dr. Daniel Moses kulola.

Sample Text

 
Blogger Templates