Sunday 21 May 2017

TAREHE RASMI YA KUANZA KWA MKUTANO WA KIMATAIFA WA OYES 2017 YAJULIKANA.

George Binagi
Tarehe rasmi ya kuanza kwa mkutano mkubwa wa kitaifa na kimataifa wa OYES (Open your Eyes and See) 2017 unaoandaliwa kila mwaka na kanisa la EAGT Lumala Mpya Jijini Mwanza imejulikana.

Mchungaji Kiongozi wa Kanisa hilo, Dkt.Daniel Moses Kulola, amebainisha kwamba mkutano huo utaanza jumamosi Mei 27 na kufikia tamati jumapili Juni 04, 2017 katika viunga vya kanisa hilo vilivyopo nyuma ya Soko Kuu la Sabasaba Jijini Mwanza.

Dkt.Kulola amebainisha kwamba waimbaji na watumishi wa Mungu kutoka ndani na nje ya nchi akiwemo Mchungaji Gary White kutoka Amerika watahudumu katika mkutano huo.

Mafundisho pamoja na mahubiri ya neno la Mungu yaliyolenga kumfungua kila mmoja ili aone Ukuu wa Mungu yatafundishwa katika mkutano huo na kama ilivyo kawaida mamia ya wananchi wanatarajiwa kufunguliwa kwenye mkutano wa OYES 2017.
 

Sample text

Welcome note

Dear our Brethren in Jesus Welcome to our website. We are so glad that you have chosen to visit our site. On this site you will be able to know us, our values and challenges as a church family, activities and our weekly and even Yearly program and what the Lord is doing through us here in EAGT Lumala mpya church , Mwanza, Tanzania. Our prayer is that as you browse through this website, the Lord will speak to you so that you may partner with us in prayer and any other way that He may lead you to. Let us join hands as we seek to fulfill the mission and vision that God has given us. Let us redeem the time, before the Lord of times returns. Again welcome. Yours in God’s service, Pastor Dr. Daniel Moses kulola.

Sample Text

 
Blogger Templates