Sunday 2 July 2017

WATUMISHI WA MUNGU KUTOKA MAREKANI WAHUDUMU EAGT LUMALA MPYA.

Mchungaji Ken Maxwell kutoka Florida Marekani akiwa na familia yake hii leo kwenye ibada za kanisa la EAGT Lumala Mpya Jijini Mwanza. Mchungaji Maxwell na familia yake pamoja na watumishi wengine wa Mungu kutoka Marekani wanaendelea kuhudumu katika kanisa hilo tangu June 27 na watafikia tamati siku ya kesho Julai 03, 2017.

Kuna ibada tatu kila jumapili, ibada ya kiingereza kuanzia saa 12 kamili hadi saa moja kamili asubuhi, ibada ya pili ya kiswahili kuanzia saa moja kamili asubuhi hadi saa nne na nusu asubuhi na ibada ya tatu ya kiswahili kuanzia saa nne na nusu asubuhi hadi saa nane kamili mchana.

Usikose kesho kuanzia saa tisa na nusu alasiri, ambapo kutakuwa na mafundisho pamoja na maombezi katika kanisa la EAGT Lumala Mpya ambapo watumishi wa Mungu kutoka Marekani pamoja na watumishi wa Mungu wenyeji kutoka kanisa hilo watakuwepo kukuhudumia kwa jina la Yesu na hakika Bwana atakubariki.
Mchungaji Ken Maxwell (kulia) na mkewe wakitoa salamu zao hii leo 
Mtumishi wa Mungu Glen Elleben kutoka Marekani
Watumishi wa Mungu Glen Elleben (kushoto) na mkewe kutoka Marekani wakisalimia kanisa hii leo
Kutoka kulia ni Mchungaji Daniel Kulola wa EAGT Lumala Mpya na Watumishi waengine  Mungu kutoka Marekani
Kutoka kulia ni Mchungaji Daniel Kulola wa EAGT Lumala Mpya International Church na mkewe pamoja na watumishi wengine wa Mungu kutoka Marekani
Mchungaji Ken Maxwell kutoka Marekani akihudumu kwenye ibada za leo kanisa la EAGT Lumala Mpya Jijini Mwanza. Kuna ibada tatu kila jumapili, ibada ya kiingereza kuanzia saa 12 kamili hadi saa moja kamili asubuhi, ibada ya pili ya kiswahili kuanzia saa moja kamili asubuhi hadi saa nne na nusu asubuhi na ibada ya tatu ya kiswahili kuanzia saa nne na nusu asubuhi hadi saa nane kamili mchana.
Moses Daniel Kulola (kulia) akiongoza ibada ya kwanza ya kiingereza ambayo huanza saa 12:00 asubuhi hadi saa 01:00 asubuhi kila jumapili
Mwimbaji wa nyimbo za injili Sam D (kulia) pamoja na George Binagi kutoks EAGT Lumala Mpya Jijini Mwanza
Wageni kutoka Marekani pamoja na waumini wa kanisa la EAGT Lumala Mpya wakifuatilia ibada za leo jumapili. Kuna ibada tatu kila jumapili, ibada ya kiingereza kuanzia saa 12 kamili hadi saa moja kamili asubuhi, ibada ya pili ya kiswahili kuanzia saa moja kamili asubuhi hadi saa nne na nusu asubuhi na ibada ya tatu ya kiswahili kuanzia saa nne na nusu asubuhi hadi saa nane kamili mchana.
Bonyeza HAPA kwa picha zaidi
 

Sample text

Welcome note

Dear our Brethren in Jesus Welcome to our website. We are so glad that you have chosen to visit our site. On this site you will be able to know us, our values and challenges as a church family, activities and our weekly and even Yearly program and what the Lord is doing through us here in EAGT Lumala mpya church , Mwanza, Tanzania. Our prayer is that as you browse through this website, the Lord will speak to you so that you may partner with us in prayer and any other way that He may lead you to. Let us join hands as we seek to fulfill the mission and vision that God has given us. Let us redeem the time, before the Lord of times returns. Again welcome. Yours in God’s service, Pastor Dr. Daniel Moses kulola.

Sample Text

 
Blogger Templates